Habari
“Wakuu wa Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini wa Sekretarieti za Mikoa Wajengewa Uwezo wa masula ya Ufuatiliaji na Tathmini Nchini”
Wakuu vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini kwa Mikoa wajengewa uwezo ili kuimarisha ufanisi katika Ufuatiliaji, Tathimini na upimaji wa Utendaji wa shughuli za Serikali katika ngazi ya Mikoa na Halmashauri ili kuweza kujipima katika utendaji wa kazi.
Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa kikao hicho kilichofanyika Mkoani Singida Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) kutoka Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali (Sehemu ya Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Bw. John Bosco Quman amesema Ufuatiliaji na Tathmini huratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuzingatia ibara ya 52 (1) (3) inayokasimu Madaraka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa msimamizi Mkuu wa Shughuli za Serikali siku hadi siku.
“Ni muhimu kuelewa dhana mbalimbali zinazohusiana na masuala ya Ufuatiliaji, Tathmini kwa kuzingatia Upimaji na Utendaji wake, pamoja na kufanya ufuatiliaji wa afua mbalimbali za Serikali zinazojumuisha; Sera, Mipango, Mikakati, Miradi na Programu zinazotekelezwa kwenye Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Halmashauri zote nchini, alieleza Bw, Quman.
Aidha Serikali inaendelea kukamiikisha Sera ya Kitaifa ya Ufuatliaji na Tathmini Nchini ambayo ipo katika hatua za Uandishi baada ya kupita katika kamati ya Kitaifa ya uchambuzi wa Sera.
Bw. Quman amesema, jitihada zinaendelea katika Mashirika ya Umma pamoja na Makampuni ya Serikali ili kuwa na Idara za Ufuatiliaji na Tathmini zinazojitegemea kama ambavyo msisitizo ulivyowekwa katika ngazi ya Mikoa na Halmshauri ili kuhakikisha vitengo hivi vinajitegemea na kutekeleza majukumu yake.




