Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA WAZIRI MKUU

Habari

Dkt. Jim Yonazi aongoza mkutano wa Tanzania National Coordinating Mechanism (TNCM)


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ambaye ni Mwenyekiti wa TNCM ameongoza Mkutano wa Tanzania National Coordinating Mechanism (TNCM) ulilenga kujadili mikakakati mbalimbali itakayoongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa Programu za Malaria, UKIMWI na Kifua Kikuu zinazofadhiliwa na Mfuko wa Dunia katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2024 hadi 2026.

Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Jengo la Tume ya Ushindani Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Aprili, 2024 na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Fedha, Wizara ya Afya, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalaum, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Medical Stores Department (MSD), Local Fund Agent (LFA), Sekretarieti ya TNCM, Asasi za Kiraia (Non State Actors - NSAs) na Wadau wa Maendeleo.

 

=MWISHO=