Habari
Dkt. Biteko awasili nchini india kwa ziara ya kikazi
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewasili nchini India kushiriki mikutano kimataifa ya nishati sambamba na Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Nishati ya India mwaka 2025 (India 3rd Annual Energy Week) kuanzia tarehe 11 hadi 14 Februari, 2025.
Katika Uwanja wa Kimataifa wa Indira Gandhi, jijini New Delhi, Dkt.Biteko amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mafuta na Gesi India, Sandeep Jain.
Wiki ya Nishati India itakutanisha Mawaziri na Watendaji Wakuu wa Sekta ya Nishati, watunga sera na wavumbuzi wa teknolojia mbalimbali za kisasa za nishati kwa lamkupata mustakabali endelevu wa upatikanaji nishati. Aidha, Wiki hiyo itahusisha maonesho ya teknolojia mbalimbali za matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia
Katika ziara hiyo, Dkt.Biteko amefustana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini pamoja na baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake wakiongozwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga.
MWISHO=