Habari
Waziri Kabudi akutana na kufanya mazungumzo na spika wa Bunge Mhe. Zungu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Profesa Palamagamba Kabudi (Mb), amekutana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), katika Ofisi ya Spika Jijini Dodoma.
Katika kikao hicho, Dkt. Jim Yonazi, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), alihudhuria na kushiriki katika mazungumzo hayo.




