Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA WAZIRI MKUU

Habari

Majaliwa kumwakilisha Rais Dkt. Samia uapisho wa Rais Rajoelina


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Disemba 15, 2023 amewasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ivato uliopo Antananarivo nchini Madagascar na kupokelewa na Waziri Mkuu wa Madagacar, Christian Ntsay.

Mheshimiwa Majaliwa kesho Disemba 16, 2023 atamwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye sherehe za kumwapisha Rais wa nchi hiyo, Andry Rajoelina  zitakazofanyika kwenye  uwanja wa Mahamasina Barea Stadium uliopo Antananarivo.

Mheshimiwa Rajoelina ameshinda nafasi hiyo kwa muhula wa tatu kwa asilimia 58.9 ya kura zilizopigwa akifuatiwa na Siteny Randrianasoloniaiko ambaye alipata asilimia 14.39 ya kura zilizopigwa

Mheshimiwa Majaliwa amefuatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje  anayeshughulikia masala ya Afrika ya Mashariki Wakili Stephene Byabato na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Eswatin  na Madagascar, Phaustine Kasike.