Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA WAZIRI MKUU

Wenye Ulemavu

KITENGO CHA WATU WENYE ULEMAVU

LENGO KUUU:


Kukuza haki na ustawi wa Watu wenye Ulemavu katika nyanja zote za maisha.

MAJUKUMU YA KITENGO CHA WATU WENYE ULEMAVU

  1. Kuandaa na kufanya mapitio ya sera, sheria na miongozo kuhusu masuala ya Watu wenye Ulemavu;
  2. kuratibu uanzishaji na uendelezaji wa programu za marekebisho na huduma za utengamao kwa ajili ya Watu wenye Ulemavu;
  3. Kuendeleza na kuratibu mipango endelevu ya uwezeshaji kwa Watu wenye Ulemavu;
  4. Kuratibu, kufuatilia, kutathmini na kufanya mapitio ya makazi, huduma na matunzo kwa Watu wenye Ulemavu;
  5. Kuratibu na kutoa huduma za ushauri kwa vyama vya Watu wenye Ulemavu na vinavyowahudumia Watu wenye Ulemavu, pamoja na mashirika ya Kitaifa na Kimataifa yanayotoa  na/au kujihusisha na huduma kwa Watu wenye Ulemavu;
  6. Kuratibu na kufanya ufuatiliaji wa utoaji wa huduma za ustawi wa jamii kwa Watu wenye Ulemavu;
  7. Kuratibu na kufanya tafiti na tathmini ya athari za afua mbalimbali kwa Watu wenye Ulemavu;
  8. Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa mikataba, itifaki na makubaliano ya kimataifa na  kikanda kuhusu haki na ustawi wa Watu wenye Ulemavu.