Habari
Watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu wajengewa uwezo uendeshaji huduma National Call Center
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) wamejengewa uwezo katika usimamizi wa mawasiliano kwa wananchi na mbinu bora za kuhudumia wananchi pamoja na matumizi ya mifumo ya kisasa ya National call centre.
Mafunzo hayo yamefanyika Jijini Dar es Salaam ambapo Muwezeshaji Bw. Willynevilline Msamo kutoka Benki ya NMB alieleza umuhimu uwezo wa kushughulikia mawasiliano kwa ufanisi na kuongeza kasi ya utoaji wa huduma ili kuhakikisha kila mwananchi anayewasiliana na taasisi anapata msaada unaostahili kwa wakati.
“Uanzishwaji na uimarishaji wa huduma za call centre, Ofisi ya Waziri Mkuu unalenga kutatua changamoto za wananchi kwa haraka kwa kuweka mfumo rahisi na wa moja kwa moja wa kupokea na kushughulikia maoni, malalamiko na mapendekezo yao,” alifafanua
Aidha huduma hii itawawezesha wananchi kupata mrejesho kwa wakati, kufuatilia masuala yao kwa ufanisi, pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma za serikali.
Bw, Msamo alisema, “hatua hii inaonesha dhamira ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya kuendelea kuboresha mifumo ya mawasiliano na kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa haraka, kwa ufanisi na kwa viwango vya juu zaidi”.




