Habari
Ndumbaro Aipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa utendaji bora
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Damas Daniel Ndumbaro, ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) pamoja na taasisi zake kwa utendaji mzuri katika kuratibu shughuli za Serikali zinazogusa maisha ya wananchi.
Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Ofisi ya Waziri Mkuu mbele ya Kamati hiyo ya Bunge.
Mhe. Ndumbaro amesema maeneo ya uratibu wa maafa na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi yanahitaji kuendelea kupewa kipaumbele ili Serikali iendelee kuwafikia wananchi kwa ufanisi.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Ummy Nderiananga, amesema Serikali imetenga fungu maalum la fedha kwa ajili ya afua za UKIMWI pamoja na kushughulikia masuala ya maafa kila mwaka wa bajeti, hatua itakayohakikisha utekelezaji endelevu wa majukumu hayo nchini.




