Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA WAZIRI MKUU

Habari

Dkt. Kilabuko: Ofisi ya Waziri Mkuu Itaendelea Kushirikiana na IFAD


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko, amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika utekelezaji wa miradi ya kilimo na uvuvi nchini. 

Ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma wakati wa kikao na ujumbe wa IFAD waliopo nchini kufuatilia utekelezaji wa mradi wa programu ya kuendeleza sekta ya Kilimo na uvuvi (AFDP). 

“Nawahakikishia kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ipo tayari kutoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuhakikisha miradi mnayoitekeleza inaleta matokeo chanya,” amesema Dkt. Kilabuko.