Home | News | Waziri Mkuu arejea kutoka Geneva
News
Speeches

Opening remarks by Rt. Hon. Mizengo P. Pinda (MP), The Prime Minister of the United Republic of Tanzania on the African Green Revolution Forum – Accra, Ghana, 2nd September, 2010...

Hotuba ya Shukrani kwa Wabunge kabla ya Mkutano wa Ishirini wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Kuvunjwa na Mheshimiwa Rais, Ukumbi wa Bunge, Dodoma, 15 Julai 2010...

More Speeches
Recently Documents

kk Quotes

kama Bunge, lakini mmoja mmoja kama watumishi wa umma, tunao wajibu mkubwa sana wa kuishi na kutenda kwa mfano. Tujiepushe na tamaa zinazoweza kuliingizia Taifa hili hasara kubwa.

Kauli ya Waziri Mkuu kuhitimisha mjadala wa Richmond,
Mkutano wa 18 wa Bunge, Februari 10, 2010
More Quotes
Videos
Photo Gallery

Bwana Dahai Gadir wa Katesh wilayani Hanang akilima kwa kutumia trejta dogo yaani Power Tiller lililotengezwa Katesh na Bw. Mohamed Elmi kwa kutumia injini ya pikipiki. Alikuwa akimwonyesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyekuwa katika ziara mkaoni Manyara Augost 13, 2009.
More Photos
Documents and Publications


mgPrint friendly version mg Email this page

Waziri Mkuu arejea kutoka Geneva

Geneva,8 October 2009

 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amerejea Dar es Salaam leo mchana (Alhamisi, Oktoba 8, 2009) kutoka Geneva ambako alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete kwenye Mkutano Mkuu wa Shirika la Mawasiliano la Kimataifa (International Telecommunication Union – ITU).
 
Akiwa Geneva, Waziri Mkuu alishiriki katika ufunguzi wa mkutano huo (Jumatatu, Oktoba 5, 2009) na kuhutubia kikao cha pamoja cha wakuu wa nchi na maofisa watendaji wakuu wa mashirika na makampuni ya teknolojia ya habari na mawasiliano duniani.
 
Katika kikao hicho cha pamoja, Mhe. Pinda alishauri kufikiria utoaji wa elimu duniani kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano ili kupunguza matumizi ya vitabu vya kawaida na  machapisho mengine.
 
Alisema matumizi kwa wingi ya vitabu na machapisho mengine yanahitaji karatasi zinazosababisha uharibifu mkubwa wa misitu na kuleta mabadiliko ya hali ya hewa yanayoiathiri dunia hivi sasa.
 
Kwenye mkutano huo Waziri Mkuu Pinda alifuatana na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Peter Msolla na Waziri wa Mawasiliano na Ujenzi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Haji Machano.
 
Mhe. Pinda pia alitembelea mabanda ya maonyesho ya mashirika na makampuni mbalimbali ya teknolojia ya habari na mawasiliano, likiwemo banda la Tanzania la Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA).
                                               
(mwisho)
Help | Disclaimer | Privacy | Site Feedback
Copyrights ©2008-2010, The United Republic of Tanzania, Prime Minister All Rights Reserved
Designed and published by DataVision International (T) Ltd