Home | News | Waziri Mkuu akabidhiwa ripoti ya Kituo cha Mabasi Ubungo
News
Speeches

Hotuba ya Mheshimiwa Mizengo P. Pinda (Mb) Waziri Mkuu Wakati wa Kufungua Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu vya Dodoma katika Ukumbi wa African Dreams – Dodoma, tarehe 25 Juni 2010...

Hotuba ya Mheshimiwa Mizengo P. Pinda (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) Kibaha tarehe 20 Juni 2010...

More Speeches
Recently Documents

kk Quotes

kama Bunge, lakini mmoja mmoja kama watumishi wa umma, tunao wajibu mkubwa sana wa kuishi na kutenda kwa mfano. Tujiepushe na tamaa zinazoweza kuliingizia Taifa hili hasara kubwa.

Kauli ya Waziri Mkuu kuhitimisha mjadala wa Richmond,
Mkutano wa 18 wa Bunge, Februari 10, 2010
More Quotes
Videos
Photo Gallery

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete kwenye Ikulu ya Chamwino, Dodoma, Februari 9, 2008.
More Photos
Documents and Publications


mgPrint friendly version mg Email this page

Waziri Mkuu akabidhiwa ripoti ya Kituo cha Mabasi Ubungo

Dodoma,28 July 2009

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amekabidhiwa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu tuhuma za ukusanyaji wa ovyo na ubadhirifu wa mapato ya Kituo cha Mabasi cha Ubungo jijini Dar es Salaam.
 
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Bw. Ludovick Utouh, alikabidhi ripoti hiyo kwa Mhe. Pinda kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu majengo ya Bunge mjini Dodoma leo mchana (Jumanne, Julai 28, 2009).
 
Akikabidhi ripoti hiyo, Bw. Utouh alisema Ofisi yake inakamilisha pia ripoti nyingine ya uchunguzi aliouagiza Waziri Mkuu kuhusu makusanyo ya mapato ya Soko Kuu la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.
 
“Hiyo ya Kariakoo tunaikamilisha, na itakuwa tayari kukabidhiwa ifikapo Agosti 15 au kabla ya hapo,” alisema Bw. Utouh.
 
Waziri Mkuu aliagiza ufanywe uchunguzi (Perfomance Audit) na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu mapato na matumizi ya makusanyo ya Kituo cha Mabasi cha Ubungo na Soko la Kariakoo ili kuboresha mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
 
Mhe. Pinda alitoa maagizo hayo alipokuwa  akiwahutubia viongozi mbalimbali wa mkoa wa Dar es Salaam katika majumuisho ya ziara yake ya siku nne ya mkoa huo Machi 15, 2009 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.
 
Katika ziara yake hiyo ya kukagua usafi na mazingira ya Jiji, Waziri Mkuu alibaini pamoja na mambo mengine, Kituo cha Mabasi cha Ubungo na Soko Kuu la Kariakoo ni maeneo mawili ambayo yangeingiza mapato makubwa kwa Jiji lakini ukusanyaji wake ni wa hovyo na kuna tuhuma za ubadhirifu.    
                                      
 (mwisho)
Help | Disclaimer | Privacy | Site Feedback
Copyrights ©2008-2010, The United Republic of Tanzania, Prime Minister All Rights Reserved
Designed and published by DataVision International (T) Ltd