November 4 2007
Wambura Chacha from Serengeti, Mara ask;
Mheshemiwa waziri mkuu naomba kuuliza wilaya ya serengeti ina kilomita za mraba elfu kumi na mia tatu lakini ina vituo viwili vya afya je serikalai ina mpango gani wa kutuongezea vituo vya afya ili kuondo kero ya wananchi kutembea umbali mrefu kupata matibabu?
Prime Minister;
Ni kweli Wilaya ya Serengeti ina kilometa za mraba 10,300 na ni kweli ina vituo vya afya viwili tu. Serikali ina mpango wa kujenga vituo vya afya katika kila kata na zahanati kwa kila kijiji. Kwahiyo mpango huu kwa kuwa utakuwa umeendeshwa Tanzania nzima kuanzia mwaka wa 2008/2009 na Serengeti ni mojawapo, kwahiyo huo ni mpango kabambe wa Serikali ili kuhakikisha kwamba huduma za afya zinatolewa katika kila kijiji na katika kila kata.
October 10 2007
Rashid Mhando from Dodoma, Dodoma ask;
Mhe. WAziri Mkuu, Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha hali ya mazingira katika stendi ya mabasi ya abiria Dodoma ?
Prime Minister;
Stendi ya Mabasi ya Dodoma, haikidhi haja kwa abiria kwani stendi hiyo ni ya muda siyo ya kudumu kwa maana ya kwamba itahamishwa. Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imeweka mikakati ya matengenezo ya Barabara zilizomo ndani ya eneo la stendi ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za ulinzi na usafi. Kwa mwaka wa fedha 2007/2008 jumla ya shilingi 14,000,000 zimetengwa kwa ajili hiyo na matengenezo ya barabara hizo na yataanza mwezi Desemba, 2007.
>> More Questions and Answers
|
|
|